1
Isaya 54:17
Swahili Revised Union Version
Kila silaha itengenezwayo juu yako haitafanikiwa, na kila ulimi utakaoinuka juu yako katika hukumu utauhukumu kuwa mkosa. Huu ndio urithi wa watumishi wa BWANA, na haki yao inayotoka kwangu mimi, asema BWANA.
Linganisha
Chunguza Isaya 54:17
2
Isaya 54:10
Maana milima itaondoka, na vilima vitaondolewa; bali wema wangu hautaondoka kwako, wala agano langu la amani halitaondolewa; asema BWANA akurehemuye.
Chunguza Isaya 54:10
3
Isaya 54:4
Usiogope; maana hutatahayarika; wala usifadhaike; maana hutaaibishwa; kwa kuwa utaisahau aibu ya ujana wako, pia masuto ya ujane wako hutayakumbuka tena.
Chunguza Isaya 54:4
4
Isaya 54:5
Kwa sababu Muumba wako ni mume wako; BWANA wa majeshi ndilo jina lake; na Mtakatifu wa Israeli ndiye Mkombozi wako; Yeye ataitwa Mungu wa dunia yote.
Chunguza Isaya 54:5
5
Isaya 54:2
Panua mahali pa hema yako, na wayatandaze mapazia ya maskani yako; usiwakataze; ongeza urefu wa kamba zako; vikaze vigingi vya hema yako.
Chunguza Isaya 54:2
6
Isaya 54:13
Na watoto wako wote watafundishwa na BWANA; na amani ya watoto wako itakuwa nyingi.
Chunguza Isaya 54:13
7
Isaya 54:8
Kwa ghadhabu ifurikayo nilikuficha uso wangu dakika moja; lakini kwa fadhili za milele nitakurehemu, asema BWANA, Mkombozi wako.
Chunguza Isaya 54:8
8
Isaya 54:7
Kwa kitambo kidogo nimekuacha; lakini kwa rehema nyingi nitakurudisha.
Chunguza Isaya 54:7
9
Isaya 54:9
Kwa maana jambo hili limekuwa kama maji ya Nuhu kwangu; maana kama nilivyoapa ya kwamba maji ya Nuhu hayatapita juu ya dunia tena, kadhalika nimeapa ya kwamba sitakuonea hasira, wala kukukemea.
Chunguza Isaya 54:9
10
Isaya 54:12
Nami nitaifanya minara yako ya akiki nyekundu, na malango yako ya almasi, na mipaka yako yote ya mawe yapendezayo.
Chunguza Isaya 54:12
Nyumbani
Biblia
Mipango
Video