Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Soma Biblia Kila Siku 03/2024Mfano

Soma Biblia Kila Siku 03/2024

SIKU 15 YA 31

Mwandishi wa waraka anakiri kwamba suala la ukuhani wa Melkizedeki kuwa mfano wa ukuhani wa Yesu, ni gumu kwa wasomaji wake kuelewa. Lakini sababu ya kutokuelewa kwao, ni uchanga wao katika imani. Tunahimizwa kujifunza zaidi neno la Mungu na kuwa tayari kukua katika ufahamu wa neno hilo. Hata leo kuna watu wa Mungu ambao shida yao ni uchanga wa imani na wa ufahamu sahihi wa neno la Mungu. Wakati mwingine sababu ni watu hao kupoteza muda wakibishana juu ya mambo yasiyo ya msingi.

siku 14siku 16

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 03/2024

Soma Biblia Kila Siku 03/ 2024 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi wa Machi pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha Waebrania. Karibu kujiunga na mpango huu

More

Tungependa kuwashukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: https://www.somabiblia.or.tz/