Soma Biblia Kila Siku 07/2025Mfano

Kila mara tunaona na kukutana na watu wanaokata tamaa. Dhiki, mateso, njaa na utumwa ni kati ya mambo yavunjayo mioyo ya watu hata leo. Lakini katikati ya hali hii itishayo kuna Mungu asiye na upendeleo. Leo tunasoma kwamba Mungu anaiongoza dunia akitumia wateule wake. Hawa wanatoka katika taifa lake. Mungu haongozi uumbaji wake kwa kutumia mataifa yenye nguvu za kiuchumi na kivita. Uchumi na vita vitakoma. Uovu haudumu. Mtu anapaswa kuweka maisha na tumaini lake kwa Mungu na si kwa watu.
Andiko
Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 07/2025 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi Julai pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha Isaya na 1 Petro. Karibu kujiunga na mpango huu
More
Tungependa kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: www.somabiblia.or.tz