Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Soma Biblia Kila Siku 07/2025Mfano

Soma Biblia Kila Siku 07/2025

SIKU 6 YA 31

Mungu anakitumia kinywa cha nabii kuleta matumaini mapya kwa watu wake na taifa zima. Ingawa watu na taifa wanazungukwa na kukabiliana na wasiomcha Mungu, wanaahidiwa jambo jipya. Ni tangazo linaloteta ahueni maishani. Katikati ya mahangaiko kuna tegemeo jipya, kwamba wale wanaowaonea na kuwatendea watu jeuri na dharau, wanakomeshwa katika udhalimu wao. Hakuna marefu yasiyo na ncha. Kile chenye mwanzo huenda mwisho. Heri wale wanaomfuata Yesu, maana wanao mwisho ulio wa baraka. Huo mwisho umetabiriwa katika Dan 7:14 kwa maneno haya: [Yesu]akapewa mamlaka, na utukufu, na ufalme, ili watu wa kabila zote, na taifa zote, na lugha zote, wamtumikie; mamlaka yake ni mamlaka ya milele, ambayo hayatapita kamwe, na ufalme wake ni ufalme usioweza kuangamizwa.

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 07/2025

Soma Biblia Kila Siku 07/2025 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi Julai pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha Isaya na 1 Petro. Karibu kujiunga na mpango huu

More

Tungependa kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: www.somabiblia.or.tz