Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Soma Biblia Kila Siku Agosti/2022Mfano

Soma Biblia Kila Siku Agosti/2022

SIKU 1 YA 31

Tumesoma jinsi mfalme Sulemani alivyoijenga nyumba yake. Hapo tunakutana na mambo makubwa mawili: Kwanza muda aliotumia kuijenga, na pili vifaa vya ujenzi vilivyotumika.Sulemani anatumia miaka 13 kuijenga nyumba yake. Hii inatufundisha kuwa tunapoamua kufanya jambo tulipe muda wa kutosha ili likamilike vizuri. Aidha anatumia mierezi, mawe ya thamani ya kuchongwa na shaba. Hii itufundishe kufanya mambo yenye kuonesha thamani na utukufu kwa Mungu. Wakristo tuondokane na kuishi maisha duni.

siku 2

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku Agosti/2022

Soma Biblia Kila Siku Agosti/2022 ni mpango wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku kwa mwezi wa Agosti pamoja na maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa kwa urahisi na kuendelea kutafakari neno la Mungu ulilosoma kwa siku husika. Katika mpango huu utasoma zaidi katika kitabu cha 1 Wafalme na Zakaria. Karibu kujiunga na mpango huu na usome bure

More

Tungependa kuwashukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz/